Monday, 23 December 2013

SERIKALI YA TANZANIA YATUNISHA MFUKO WA WACHIMBAJI MADINI WADOGO






Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Profesa Sospeter Muhongo akiongea na washiriki wa  mkutano mkuu wa mwaka wa wachimbaji wadogo wa madini uliofanyika hivi karibuni mjini Dodoma.
------------------------------------------

Jamhuri ya Muungano Tanzania kupitia Wizara ya Nishati na Madini imetenga jumla ya shilingi bilioni 8.9 kwa ajili kuwainua wachimbaji wadogo wa madini nchini
ili kuwawezesha katika shughuli zao za uchimbaji wa madini. 

Serikali katika  jitihada za kuwainua wachimbaji wadogo zinalenga pia kuinua pato la taifa kutokana na kuongezeka kiwango cha kodi na tozo mbalimbali zinazopaswa kulipwa na wachimbaji hao kwa serikali.

Akizungumza na wajumbe waliohudhuria mkutano mkuu wa mwaka wa wachimbaji wadogo wa madini nchini, uliofanyika mjini Dodoma hivi karibuni,  

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo alisema

“Tunayo dhamira ya dhati kuwasaidia ili maisha yenu yaboreke na pia ili kukuza pato la taifa hili”, alisisitiza Waziri Muhongo na kuongeza kuwa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) ndilo limepewa jukumu la kusimamia mipango ya uendelezaji wachimbaji wadogo kwa kushirikiana na taasisi nyingine mbalimbali zinazohusika na sekta ya madini.

Ili kufanisha  zoezi hili  Profesa Muhongo amewataka wachimbaji wadogo wa madini nchini kuhakikisha wanasajili biashara zao, kuanisha mapato yao, pamoja na kulipa kodi na tozo mbalimbali zinazowahusu ili taifa liweze kunufaika na rasilimali hiyo ya madini. 










No comments: