Friday, 28 February 2014

TOTAL YAZINDUA AWANGO KUMALIZA TATIZO LA UPATIKANAJI WA UMEME KWA WATU WA KIPATO CHA CHINI TANZANIA.

 


Mgeni Rasmi, Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akihutubia wageni rasmi (hawapo pichani) waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa AWANGO uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency,jijini Dar es salaam,usiku wa jana.Waziri Muhongo aliwapongeza TOTAL kwa juhudi wanazozifanya  kusaidia jamiii ya watanzania  kupata chnzo cha Nishati  kitakachowaletea  maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Pembeni ni baadhi ya bidhaa hizo zinazotumia nishati ya jua.






Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo (kulia),Mgeni rasmi katika uzinduzi wa bidhaa zinazotumia Nishati ya jua kuzalisha umeme  zinazojulikana kama AWANGO,wa kwanza kushoto ni Balozi wa Ufaransa nchini nTanzania Mh Marcel Escure pamoja na Mkurugenzi mkuu wa TOTAL nchini Tanzania Bw.Stephane Gay wakishuhudia tukio mojawapo katika hafla hiyo.






Meneja wa Maswala ya Kisheria Bi Marsha Msuya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa AWANGO zilizo  chini ya mradi wa TOTAL unaojulikana kama ‘’Total Access to Solar’’ (TATS) wenye  lengo la kutatua tatizo la ukosefu wa umeme nchini Tanzania kwa jamii ya watu wa kipato cha chini wakiwa na malengo ya kuhakikisha bidhaa hizo zinafika mikoa yote ya nchi nzima. 

Source: Michuzi Blog.

No comments: