Wednesday, 5 March 2014

HISTORIA YA UVUMBUZI WA MADINI YA TANZANITE NCHINI TANZANIA







Mzee Jumanne Mhero Ngoma (Mvumbuzi wa Madini Pekee duniani
yanayopatikana nchini Tanzania)

Historia ya Mvumbuzi
Jumanne Mhero Ngoma, Mtoto Wa Mfugaji. Alizaliwa Katika Kijiji Cha Marwa, Wilaya Same Mkoa Wa Kilimanjaro, Wazazi Wake Walihamia  Mererani Wakitokea Kijiji Cha Marwa Kwa Ajili Ya Kutafuta Malisho Ya Mifugo Yetu.

Alipokuwa Mdogo, Alikuwa Akimsaidia Baba Yake Kuchunga Mifugo Yao Wakati Wa Likizo.

Kama Ilivyo Kawaida Kwa Watoto Wadogo Kupenda Kucheza, Nilipokuwa Porini Nilikuwa Nachezea Mawe Ambayo Yalinivutia Kwa Rangi Zake, alikuwa akiyapanga kutokana Uwepo Wa Rangi Zake Tofauti Na Kuyapa Majina Ya Mifugo yao. Sehemu Hasa Niliyokuwa Nayapata Mawe Haya Inajulikana Kama Kijiji Cha Nyaisunyae.

Mzee Ngoma alipata Elimu Yangu Ya Awali Town School Iliyopo Mkoani Arusha Na Kufaulu Kujiunga Mringa Middle School Mkoani Arusha Ambapo hakubahatika Kumaliza Kutokana Na Kufariki Baba Yangu Na Kukosa Mtu Wa kumlipia Ada.

Baada Ya Kushindwa Kuendelea Na Elimu Yangu Ya Middle School Nilirudi Pale Mererani Kuendelea Kuchunga Mifugo Ya Baba yake Japo Nilikuwa Bado Na Mwamko Na Ari Wa Kuendelea Na Kupata Elimu.

Mwaka 1966 aliabahatika Kwenda Kusoma Morogoro Chuo Cha Madini Kwa Muda Wa Miezi Mitatu, Baada Ya Kupata Msaada Wa Kaka yake Ambaye Wakati Huo Nae Alikuwa Akifanya Kazi Ya Udereva. Alipokuwa Chuoni Chini Ya Mwalimu wake Aliyekuwa Akiitwa Mkali Dachi  Alimsaidia Sana Kupata Utaalam Wa Mambo Ya Madini.  Mara Baada Ya Kumaliza Chuo Na Kupata Elimu Ya Madini, June 1966, Alibahatika Kupata Leseni yake Ya Uchimbaji Wa Madini,  Alirudi Mererani, alipofika Mererani aliamua Kuchukua Yale Mawe Ambayo Nilikuwa anachezea Japo Yalikuwa Tofauti Sana Na Aina Ya Madini aliyofundishwa Pale Morogoro, Aliamua Kuyachukua Na Kuyapeleka  Moshi Office Ya Madini Wakati Huo Mwanzoni Mwa Mwaka 1967 Ili Yaweze Kufanyiwa Utafiti Kuwa Yalikuwa Mawe Gani. alibahatika Kuonana Na Afisa Wa Madini Bwana Bills. Kwa Bahati Mbaya Nae Alishindwa Kuyatambua Japo Yalimvutia Sana Na Kujaribu Kuyafananisha Na Madini Ya Blue Tourmaline Baada Ya Majadiliano Nae walikubaliana Ayapeleke Office Madini Dodoma Kwa Utafiti Zaidi.

Baada Ya Uchunguzi Wa Maabara Ya Madini Dodoma, Mnamo Septemba 1967 Majibu Yalitoka Na Kuonyesha Kuwa Ni Madini Jamii Ya Zoisite, Na Kushauri Kuwa Kwa Kipindi Hicho Hayakuwa Na Soko Japo Soko Linaweza Kuwepo Baadae.

Uchunguzi Mwingine Zaidi Uliohusisha Ofisi Nyingine Za Serikali Ambapo Mwaka 1984,  Pro. Simon Mbilinyi Mshauri Wa Uchumi Ofisi Ya Rais Kipindi Hicho, Alithibitisha Kuwa Mgunduzi Wa Madini Ya Tanzanite Ni Bwana Jumanne Mhero Ngoma. Rais Alikubali Kwa Maandishi Akaamuru Apewe Tuzo Na Cheti Cha Utambuzi 


……………………..Endelea Kufuatilia, historia yake inaendelea………………………..

1 comment:

Unknown said...

God bless you Mr ngoma