Wednesday, 21 May 2014

WADAU WA UONGEZAJI THAMANI MADINI WAFANYA MKUTANO JIJINI DAR

Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni Bw. Celestine Onditi wa pili kulia amabaye alikua mgeni rasmi katika mkutano wa wadau wa ukusanyaji maoni sheria ya uongezekaji thamani madini akiwa katika picha ya pamoja na wadau hao. Wakwanza kushoto ni kamishna msaidizi wa sheria ya uongezaji thamani madini, mhandisi  Hamisi Komba,(wa tatu kushoto) ni kamishna msaidizi wa uchumi na biashara mhandisi Salim  Salim, kamishna msaidizi wa madini kanda ya kusini mhandisi Benjamin Mchwampaka wa kwanza kulia ni kamishna msaidizi wa kanda magharibi Shubi Byabota.


Mhandisi madini na uchenjuaji migodi Wizara ya Nishati na Madini, Bi. Asnath Mkani akiwasilisha mada ya historia ya uongezaji thamani madini nchini.

Baadhi ya wadau wa sheria ya uongezaji thamani madini wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa mkutano huo.

Katibu tawala wa Wilaya ya Kinondoni Bw. Celestine Onditi akisalimiana na baadhi ya wadau wa sheria ya uongezaji thamani madini mara baada ya kufungua mkutano huo.

                    Na Hamisi Yassn, Dar es salaam

Katika picha ni mkutano wa wadau wa sheria ya uongezaji thamani madini unaoendelea jijini dar es salaam baada ya mkutano kama huo uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Arusha. Mikutano hiyo inafanyika ili kupata maoni ya wadau wa tasnia ya madini ya vito na usonara kwa ajili ya rasimu ya sheria hiyo.


Wakati akifungua mkutano huo jana, katibu tawala wa Wilaya ya Kinondoni  Bw. Celestine Onditi aliwataka wadu kutoa maoni yao ili iweze kupatikana sheria ambayo itakuwa ni shirikishi akiunganisha maoni ya wadau wote wa sekta ya madini hali itakayo saidia. Ameongeza endapo wadau watatoa maoni  stahiki sheria hiyo itasaidia sekta ya madini kuchangia kwa pato la Serikali kwa kiasi kikubwa zaidi ikizingatia kuwa nchi ya Tanzania imebarikiwa kuwa na hazina kubwa ya madini ya aina mbalimbali.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mgesa Mulongo wakati akifungua mkutano kama huo jijini Arusha aliwataka wadau wa sheria kutoa maoni yatakayosaidia sheria hiyo kuwa yenye tija kwa manufaa ya taifa na Watanzania.

3 comments:

Unknown said...
This comment has been removed by the author.
Unknown said...
This comment has been removed by the author.
Unknown said...

ni vizuri kuona wadau wanakutaka kujadili maendeleo ya madin pamoja na kuyatungia sheria kwa manufaa ya yaifa