Kampuni zinazomiliki migodi mikubwa na ya kati
nchini zimeendelea kulipa stahiki mbalimbali za Serikali, ikiwa ni
pamoja na kodi ya mapato.
Katika kuonyesha kwa vitendo, Wakala wa Ukaguzi wa
Madini Tanzania (TMAA) imetoa rekodi inayoonyesha walivyolipa kodi
katika kipindi cha Mei hadi Novemba 2013.
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri (TMAA), Dk Yamungu
Kayandabila anasema Kampuni ya Resolute Tanzania inayomilikiwa na
mgodi wa dhahabu wa Golden Pride imelipa kodi ya mapato ya Sh6.1
bilioni.
Dk Kayandabila anasema fedha hizo ni kodi ya
mapato ambayo imefikisha jumla ya Sh97 bilioni tangu kampuni hiyo
ilipoanza kulipa kodi ya mapato mwaka 2010.
Anasema kwa upande wa kampuni ya dhahabu ya Geita
imelipa Sh4.8 bilioni na kufikisha jumla ya Sh304.2 bilioni tangu
ilipoanza kulipa kodi ya mapato ya mwaka 2009.
Dk Kayandabila anasema kampuni ya almasi ya
Williamson imelipia Sh178.9 milioni kama altenative minimum tax na
malipo hayo yalifanyika kwa mujibu wa sheria ya kodi ambayo inataka
mlipa kodi anayepata hasara kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo
kulipa aina hiyo ya kodi ambayo hutozwa kwa kukokotoa asilimia 0.3 ya
mauzo ya kipindi husika.
Mgodi wa Tuwalawaka unaomilikiwa na ABG haukulipa
kodi ya mapato katika kipindi hiki kutokana na mdororo wa bei ya dhahabu
na mgodi huo ulifungwa rasmi Julai 30, mwaka huu. Jumla ya kodi ya
mapato ambayo imewahi kulipwa na kampuni hiyo wakati wa uhai wake ni
Sh77.4 bilioni.
“Malipo mbalimbali yaliyoyolipwa serikalini na
migodi baada ya kubainika kutolipwa. Ukaguzi uliofanywa na TMAA
imefanikiwa kukusanya jumla ya Sh3.46 bilioni ambazo zimelipwa
serikalini.
Baadhi ya wamiliki wa migodi mikubwa na ya kati
iliyokaguliwa katika kipindi cha Mei hadi Novemba, 2012, malipo hayo
yanajumuisha mrabaha, kodi ya zuio na nyingine stahiki,” anabainisha Dk
Kayandabila.
Anasema Serikali imepata mrabaha na takwimu sahihi
za madini yanayozalishwa na migodi mikubwa nchini baada ya TMAA kufanya
ukaguzi wa uzalishaji na mauzo kwenye migodi mikubwa ya dhahabu ya
Geita, Golden Pride, Bulyanhulu, Buzwagi North Mara, Tulawaka na New
Luika.
Anaeleza kwamba pia kaguzi zinaendelea kufanyika katika mgodi wa almasi wa Mwadui, mgodi wa TanzaniteOne uliopo Mirerani
Source : mwananchi communication
No comments:
Post a Comment